"Zana zote za biashara mahali pamoja — kwa vijana wa Tanzania"
All Business Tools Under One Roof
Powered by Mummy Jacky's Business Academy · Dar es Salaam, Tanzania
4
Zana Kuu
11+
Kikokotoo
30+
Mada za Mwongozo
100+
Bidhaa za Kariakoo
Mummy Jacky's Business Academy
Zana 5 za Biashara & Maisha
Zana zinazokusaidia kuandika, kupanga, na kufanya maamuzi ya biashara — kwa Kiswahili, kwa vitendo, bila mshauri wa gharama.
💡TZS 3,000
Mawazo ya Biashara
Sijui biashara ya kufanya. Ninahitaji mawazo 10 yanayofaa mtaji wangu, eneo langu, na ujuzi wangu — sasa hivi.
Chagua Zana Hii →
📋TZS 5,000
Business Plan ya Haraka
Nina biashara yangu. Nahitaji business plan kamili ya kitaalamu kwa benki, wawekezaji, au kumbukumbu yangu.
Chagua Zana Hii →
📄TZS 5,000
Business Proposal ya Haraka
Nataka kutoa proposal kwa mteja, shirika, au mfadhili wa mradi wangu. Inahitajika kuwa ya kitaalamu.
Chagua Zana Hii →
🧭TZS 3,000
Ushauri wa Biashara
Nina swali maalum la biashara. Nataka jibu la kina la vitendo — sio la vitabu, bali halisi kwa Tanzania.
Chagua Zana Hii →
🌟TZS 5,000 · Maswali 20
Tathmini ya Wito Wako Katika Maisha
Maswali 20 ya kukusaidia kujua njia yako bora — kazi, biashara, au kujiajiri. Ripoti kamili ya kibinafsi inayobainisha nguvu zako, njia yako, na hatua zako za kwanza.
Chagua Zana Hii →
Zana Zetu
Kila kitu unachohitaji kuendesha biashara yako
Tatizo kubwa la ukosefu wa ajira kwa vijana wa Tanzania halitaishia tu kupata kazi — jibu ni kuwa mmiliki wa biashara yako mwenyewe. Tunakupa zana, maarifa, na mwongozo unaohitajika kuanza, kukua, na kufanikiwa.
🔢
02 · Kikokotoo cha Biashara
Zana 11 za Hesabu za Biashara
Hesabu sahihi za bei, faida, mtaji wa kuanzia, mzunguko wa pesa, break-even, mkopo, stoki, mishahara, mauzo ya siku, akiba, na bajeti binafsi. Zana 11 zote kwa Kiswahili na Kiingereza — na ripoti za kina kwa TZS 2,000 kila moja.
Bei & FaidaMkopoCash FlowBajeti Binafsi
📚
03 · Mwongozo wa Biashara
Ensaiklopidia ya Biashara Tanzania
Makala zaidi ya 100 yanayoshughulikia changamoto za biashara kutoka mwanzo hadi ukuaji — jinsi ya kuanza, mtaji, masoko, wateja, ushindani, dijitali, kodi, wafanyakazi na zaidi. Kila makala ina hatua za vitendo, mifano halisi kutoka Tanzania, na mpango wa siku 7.
30+ MadaHatua za VitendoMfano wa TanzaniaMpango wa Siku 7
🛒
04 · Machimbo ya Kariakoo
Dira ya Vyanzo vya Bidhaa — Dar es Salaam
Tafuta chanzo cha bidhaa yoyote unayotaka kuuza — nguo, chakula, teknolojia, vifaa vya ujenzi, mazao ya kilimo, na zaidi. Kwa kila bidhaa utapata mahali pa kununulia, bei ya wastani ya jumla, mtaji unaohitajika, na makosa ya kuepuka. Bidhaa zaidi ya 100.
100+ BidhaaBei za JumlaMitaa ya Kariakoo
Dhamira Yetu
Kwa Nini Zana za Biashara?
Ukosefu wa ajira kwa vijana wa Tanzania haufumbuliwi kwa kuomba kazi peke yake. Jibu lake ni ujasiriamali — lakini ujasiriamali unahitaji maarifa, zana, na mwongozo sahihi. Hiyo ndio tunayotoa hapa.
🎯
Mwongozo wa Vitendo — Si wa Vitabu
Hatutoi nadharia. Kila zana, kila makala, kila kikokotoo imeundwa kuhusu mazingira halisi ya biashara Tanzania — bei za TZS, masoko ya mtaa, na changamoto za kila siku ambazo unazijua vizuri.
🇹🇿
Kwa Kiswahili — Lugha ya Uelewa Wako
Elimu ya biashara inagusa moyo zaidi ukisikia kwa lugha unayoielewa vizuri. Zana zetu zote zimejengwa kwa Kiswahili — hii ndiyo nguvu yetu kubwa. Hakuna lugha ya kizuizi kati yako na maarifa yako.
🚀
Fanya Uamuzi Sahihi — Kuanzia Leo
Hesabu faida kabla ya kununua bidhaa. Jua bei ya break-even yako. Pata chanzo cha bidhaa yako. Andika business plan kwa dakika chache. Zana hizi zinakupa nguvu ya kuamua kwa ujuzi — si kwa nadhani.
Wasiliana Nasi
Tuko Goba, Dar es Salaam — tayari kukusaidia kwa simu, WhatsApp, au barua pepe. Usisimame peke yako.